Wednesday, 12 May 2021

SIMBA FC YATUA KIBABE SOUTH AFRICA...

Hii ni baada ya tarehe kuwa zimekaribia (15.05.2021) kwa Timu nane bingwa Afrika kuchuana katika kutimiza hatua ya Robo Fainali ya Club Bingwa Africa, Simba Sport Club, kama ilivyo ada teari wameshawasili South Africa kwaajili ya kuvaana na wataalamu wa soka nchini humo Kaizer Chiefs.

Simba kibabe kabisa jana waliondoka nchini jumla ya wachezaji 24 pamoja na benchi la ufundi bila kuwa mbali na msemaji mkuu wa timu hiyo gwiji wa mpira kwa sasa nchini Tanzania Bw.Haji Manara. Uongozi wa Simba FC umeviambia vyombo vya habari mbali mbali kwamba kuna mambo kadha wa kadha dhidi ya nyota wa soka la mpira wa miguu Benard Morrison ambayo yanaendelea kuwekwa sawa na muda wowote ataanza safari kuelekea south africa ili kuhakikisha wanakuwa na mwanzo mzuri wa hatua hii ya Robo fainali Club Bingwa Arica.

Mungu Ibariki Simba, Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Africa Mashariki!

No comments:

Post a Comment